CCM Yaipongeza SUA kwa Utekelezaji wa Miradi kwa Vitendo

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo amekipongeza Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa utekelezaji wa Miradi kwa vitendo na kuwataka kuanzisha mfumo mzuri utakaowezesha kupata vijana ambao hawafikirii kuajiriwa bali kujiajiri ili waajiri wengine kwa kuwa ndiyo njia pekee ya kulifanya Taifa kufikia malengo yake ya kumkwamua mwananchi wa kawaida ambaye maisha yake yanategemea Kilimo.

CCM Yaipongeza SUA kwa Utekelezaji wa Miradi kwa Vitendo

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo akizungumza na wafanyakazi na wanafunzi wa SUA (hawapo pichani) wakati wa ziara yake kujionea Miradi ya Maendeleo chuoni hapo

Chongolo amesema hayo Februari 5, 2023 wakati alipotembelea Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa Chuoni hapo na kuzungumza na Wafanyakazi pamoja na Wanafunzi katika ukumbi wa ‘Multipurpose’ Kampasi ya Edward Moringe Sokoine mkoani Morogoro.

Chongolo amesema lazima kuwepo na  lengo la kuzalisha watu ambao  wakiondoka wataenda kuwa wawakilishi wazuri  kwa maana ya kutengeneza matokeo zaidi katika eneo lao la Taaluma hivyo nchi  inahitaji kuwa na taaluma zinazoipeleka kwenye uzalishaji wa moja kwa moja kwa kiwango cha juu na SUA  ikiwa katika njia hiyo ya uzalishaji nchi itakuwa na chakula cha kutosha kuliko sehemu nyingine Afrika na duniani kwa ujumla

IMG 0403.CR2  0

Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Prof. Raphael Chibunda (aliyeshika kipaza sauti) akitoa maeelezo kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo wakati wa ziara chuoni hapo

Aidha amesema asilimia 80 ya Watanzania ni Wakulima na kutokana na hali hiyo wanakuwa wadau wakubwa wa SUA kwa asilimia 100, mdau huyo anatakiwa kuwa na uelewa wa kutosha juu ya kile anachokifanya na nchi hii inawaangalia wasomi hususani katika kumtoa mkulima kutoka kwenye kulima kawaida na kwa ajili ya tumbo kwenda kulima kibiashara kwa maendeleo yake binafsi na Taifa kwa ujumla.  

‘‘Mimi nimebahatika kuwa nakuja sana SUA kufuata miche ya Miti kwa sababu maisha yangu ni Kilimo, niwe mkweli nimeona mabadiliko makubwa sana na ya kweli ambayo yanahitaji utashi tuliopewa na Mwenyezi Mungu kusogeza kijiti ili mambo yaende nje na kutokea kuwa makubwa na naamini kupitia utaalamu nilioendelea kujifunza SUA  mabadiliko yatakuwa makubwa sana na kwenda kunufaika zaidi kwa kile ninachokiamini”, amesema Daniel Chongolo

IMG 0300.CR2

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo (wa tatu kutoka kulia) akisikiliza maelezo ya uzalishaji wa mazao ya mbogamboga katika Atamizi iliyopo SUA ( wa nne kutoka kushoto) ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bibi. Fatma Mwasa

Kwa upande wake Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Raphael Chibunda ameishukuru Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kukipatia Chuo kiasi cha shilingi Bilioni 73.6 sawa na Dola za Kimarekani Milioni 32.6 kupitia Mradi wa 'Higher Education for Economic Transformation' (HEET) ambapo wameahidi kwenda kutumia fedha hizo kujenga na kupanua miundombinu mipya katika Kampasi zao za mafunzo yaani Edward Moringe, Solomoni Mahlangu na Mizengo Pinda.

Aidha, amesema Chuo kitaenda kuboresha mitaala yake ili iweze kuakisi mahitaji ya Soko la Ajira kwa kununua Vifaa vya kisasa vya Mafunzo pamoja na kupeleka wafanyakazi katika Mafunzo hivyo kupitia Mradi huo wataenda kutekeleza kwa nguvu zao zote na uadilifu mkubwa kwa kuhakikisha waliyoyapanga  yanaenda kutokea kweli

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo alikuwa na ziara ya siku tisa (9) Mkoani Morogoro ambapo ilianza Januari 27 , 2023 na kuhitimishwa Februari 5, 2023 siku ya Kilele cha Maadhimisho ya Miaka 46 ya Chama cha Mapinduzi (CCM) tangu kuanzishwa kwake mwaka 1977

IMG 0530.CR2  0

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo (aliyevaa kofia) akipokea zawadi ya mboga, viungo na matunda kutoka kwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Prof. Raphael Chibunda (wa pili kulia)

IMG 0557.CR2

IMG 0476.CR2

IMG 0448.CR2

IMG 0345.CR2

Pichani hapo juu ni matukio mbalimbali ya ziara ya  Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo

 

 

Na; Winfrida Nicolaus

Picha zote na Gerald Lwomile

Share this page