Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amewataka Wataalamu wa Misitu kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kuhimiza utekelezaji wa utunzaji na uendelezaji wa misitu nchini kwa manufaa ya vizazi vya sasa na baadaye.
Amebainisha hayo katika siku ya kufunga Maadhimisho ya Miaka 50 ya kuanzishwa kwa Kitivo cha Mafunzo ya Misitu katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) ambapo amesema kitu wanachotakiwa kukifanya ni kuendelea kutoa elimu kwa jamii ili kuisadia kupata uelewa wa umuhimu wa uhifadhi wa Misitu katika maeneo yote kwa ajili ya kukiwezesha kizazi kijacho kuja kunufaika na misitu na mazingira kiujumla.