Rais Samia azindua Jengo Mtambuka la Mafunzo SUA, akimwagia sifa Chuo kwa kufanya vizuri
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua Jengo Mtambuka la Mafunzo lililopo katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) na kukipongeza Chuo hicho kwa kufanya tafiti zenye tija nchini na kutoa majibu kwa mahitaji ya jamii za Tanzania na Afrika.