Wanasayansi watakiwa kufanya tafiti zinazotatua matatizo ya jamii na zilenge mapinduzi ya nne ya viwanda yajayo

Ushauri huo umetolewa na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma utafiti na ushauri wa Kitaalamu Prof. Maulid Mwatawala wakati akifungua mafunzo ya siku nne kwa wanataaluma wachanga wa Chuo hicho juu ya namna ya kuandika maandiko kwaajili ya kuomba fedha za kufanya tafiti.