Intensification of cooperation with Mzumbe and Sokoine University of Agriculture, Tanzania

The ERASMUS cooperation with two universities in Tanzania was intensified as Dr. Simone Giertz, international coordinator at the Depratment of Geography, University of Bonn, visited both universities in May. In June, Prof. Felister Mombo from Sokoine University of Agriculture (SUA) and Dr. Lucy Massoi from Mzumbe University visited Bonn.

Msitu wa Hifadhi wa Mazumbai Wawezesha Watafiti na Watalii Duniani

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimeendelea kupokea Watafiti, Wanasayansi na Watalii kutoka nchi mbalimbali duniani wanaokwenda kujifunza, kufanya tafiti na utalii juu ya masuala mbalimbali ya Misitu na Viumbe wengine wengi kwenye Msitu wa Hifadhi Mazumbai ambao haujawahi kuguswa toka miaka ya 1,800 enzi za ukoloni wa Mjerumani. Msitu huu unapatikana Jimbo la Bumbuli Mkoani Tanga. Hayo yamebainishwa na Mhadhiri Msaidizi na Kaimu Mwangalizi wa Msitu huo na kituo hicho cha Mafunzo cha SUA Mhifadhi Chamalindi Bugingo Muriga wakati akiongea na Waandishi wa habari waliokwenda kutembelea kituo hicho kuona vivutio mbalimbali vya kipekee na viumbe vinavyopatikana kwenye msitu huo.

SUA Yafanya Makubaliano ya Ushirikiano na Taasisi za Nchini India

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimekubaliana kuweka ushirikiano na Taasisi za nchini India ikiwemo Taasisi ya Teknolojia India (ITI) katika maeneo mbalimbali ikiwemo Tafiti zinazohusu matatizo yanayokabili nchi hizo, Makampuni ya kibiashara, kupeleka Wanataaluma na Wafanyakazi kwenye mafunzo katika vyuo vikuu vya India ili kuweza kupata utatuzi wa changamoto zinazozikabili nchi hizo pamoja na watu wake.