COSTECH Yatoa Mil. 480 kwa WATAFITI Wanne
SERIKALI kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), imetoa sh milioni 480 kwa watafiti wanne kutoka Vyuo Vikuu hapa nchini kwa ajili ya kutekeleza miradi waliyoomba.
Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH, Dkt Bugwesa Katale alieleza hayo wakati wa kukabidhi mfano wa hundi kwa watafiti hao baada ya kupewa mafunzo na COSTECH.