Msitu wa Hifadhi wa Mazumbai Wawezesha Watafiti na Watalii Duniani
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimeendelea kupokea Watafiti, Wanasayansi na Watalii kutoka nchi mbalimbali duniani wanaokwenda kujifunza, kufanya tafiti na utalii juu ya masuala mbalimbali ya Misitu na Viumbe wengine wengi kwenye Msitu wa Hifadhi Mazumbai ambao haujawahi kuguswa toka miaka ya 1,800 enzi za ukoloni wa Mjerumani.
Msitu huu unapatikana Jimbo la Bumbuli Mkoani Tanga.
Hayo yamebainishwa na Mhadhiri Msaidizi na Kaimu Mwangalizi wa Msitu huo na kituo hicho cha Mafunzo cha SUA Mhifadhi Chamalindi Bugingo Muriga wakati akiongea na Waandishi wa habari waliokwenda kutembelea kituo hicho kuona vivutio mbalimbali vya kipekee na viumbe vinavyopatikana kwenye msitu huo.