SUA na NEMC Yapanda Miti Zaidi ya 45,000 katika Vyanzo vya Maji Nyanda za Juu Kusini
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uhifadhi wa Mzingira (NEMC) wamepanda miti rafiki na maji zaidi ya 45,000 kwenye vyanzo vya maji vya Mto Mbarali unaochangia maji yake kwenye Mto Ruaha Mkuu, Bwawa la Kidatu na Bwawa la Mwalimu Nyerere kama sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutunza vyanzo vya maji nchini.