Maadhimisho ya siku ya nyuki duniani yalifanyika kitaifa mkoani Singida, katika viwanja vya Bombadia. Maadhimisho hayo yaliambatana na maonesho yaliyoanza tarehe 18/5/2023 na kufikia kilele chake tarehe 21/5/2023. Wadau mbalimbali walihudhuria maadhimisho hayo, ikiwemo wawakilishi kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Kampasi ya Mizengo Pinda. Kampasi hiyo ni mdau muhimu sana kwa kuwa inatoa Shahada ya Usimamizi wa Rasilimali za Nyuki. Maadhimisho ya mwaka huu yalikua na kaulimbiu isemayo, “Tuwalinde Nyuki kwa Ustawi wa Mazingira na Usalama wa Chakula.”