Nane Nane 2022: Rai yatolewa kwa Serikali tafiti za SUA zipewe kipaumbele
Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Peter Pinda ametoa rai kwa Serikali kuhakikisha wanazipa kipaumbele Tafiti zinazofanywa na Vyuo vikuu Tanzania ikiwemo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kila Mwaka ili kuisaidia jamii na kuleta Maendeleo kwa Taifa.