Nane nane 2022: SUA yatoa Elimu ya matumizi endelevu ya misitu
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kupitia Ndaki ya Misitu, Wanyamapori na Utalii imeendelea kutoa elimu kuhusiana na ukuzaji, utunzaji na matumizi endelevu ya misitu hasa upande wa vitu ambavyo vinaathiri kwa namna hasi uoto wa asili au misitu lengo likiwa kutunza uoto wa asili kwa matumizi endelevu ya misitu nchini.