MAKISATU 2022: Serikali yaahidi kuendelea kuwekeza kwenye ubunifu nchini

Mashindano haya ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa Serikali wa kuimarisha na kuendeleza teknolojia na maarifa asilia ya ndani ili yaweze kuchangia katika uchumi wa nchi. MAKISATU yanafanyika kila mwaka na yanahusisha wabunifu kutoka makundi ya Shule za Msingi, Sekondari, Vyuo vya Ufundi Stadi, Vyuo vya Kati, Vyuo Vikuu, Taasisi za Utafiti na Maendeleo na Mfumo usio Rasmi.