Majani ya JUNCAO kuwa suluhisho la malisho ya mifugo

Wafugaji nchini Tanzania wametakiwa kuanza kulima majani aina ya JUNCAO yanayozalishwa katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kutokana na majani hayo kuonekana kuwa na faida nyingi kwa mifugo na uwezo wake wa kukua haraka na kuvumilia ukame na hivyo kupunguza changamoto za malisho wakati wa kiangazi na kumaliza migogogo ya wakulima na Wafugaji.

Tathlitha ya kumi na mbili ya Baraza

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo Prof. Raphael Chibunda amemshukuru Mwenyekiti wa Baraza Mhe. Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Chande Othman pamoja na wajumbe wote kwa kazi Kubwa na nzuri waliyoifanya na ushirikiano waliouonesha katika kusaidia mafanikio ya Chuo na utekelezaji wa majukumu ya Chuo kwa ufanisi.