Nane nane 2022: Wafugaji washauriwa kuwekeza kwenye ufugaji wa samaki
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kupitia Ndaki ya Kilimo, Idara ya Sayansi ya Wanyama, Viumbe Maji na Malisho imeshauri jamii hususani wakulima na wafugaji kuwekeza kwenye ufugaji wa Samaki kwa kuwa ufugaji wa samaki kwa sasa una soko kubwa na umekuwa ni chanzo cha ajira kwa watu wengi.