Mradi wa Cystnet Afrika Wawasilisha Matokeo ya Utafiti wa Minyoo Tegu ya Nguruwe Tanzania
Watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA, Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Taasisi ya Utafiti wa magonjwa ya Binadamu NIMR, wamefanya utafiti na kuja na mapendekezo yatakayowezesha kumaliza tatizo la minyoo tegu ya Nguruwe ambayo ina madhara makubwa kwa afya ya Binadamu na Wanyama.