Mradi wa Cystnet Afrika Wawasilisha Matokeo ya Utafiti wa Minyoo Tegu ya Nguruwe Tanzania

Watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA, Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Taasisi ya Utafiti wa magonjwa ya Binadamu NIMR, wamefanya utafiti na kuja na mapendekezo yatakayowezesha kumaliza tatizo la minyoo tegu ya Nguruwe ambayo ina madhara makubwa kwa afya ya Binadamu na Wanyama.

Serikali kushirikiana na SUA kutunza eneo la Utalii wa Kihistoria

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Pauline Gekul amesema serikali kupitia Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika itaendelea kushirikiana na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kuyaendeleza, kukarabati na kutunza kumbukumbu zote za kihisitoria  zilizoachwa na wapigania uhuru wa Afrika ya Kusini katika eneo la Kampasi ya Solomon Mahlangu.

Matokeo ya Utafiti ya Mradi wa FoodLAND Kusaidia Kuboresha Kilimo na Lishe Afrika.

Imeelezwa kuwa matokeo yote mazuri ya Mradi wa Chakula Kilimo na Lishe (FOODLAND) yaliyopatikana kwenye nchi zinazotekeleza mradi huo yatakwenda kuisaidia jamii katika kuhusanisha Kilimo, Matumzi ya mazao ya chakula na lishe na hivyo kupunguza changamoto za chakula na lishe Afrika. Kauli hiyo imetolewa na Naibu Makamu Mkuu wa Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA)  upande wa Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu Prof. Maulid Mwatawala wakati akifungua Mkutano Mkuu wa wa tatu wa Mwaka wa Mradi huo uliofanyika visiwani Zanzibar wa kufanya tathimini ya kazi zilizofanyika ndani ya mradi ili kuendelea kuboresha ufanyaji kazi wa mradi huo.