SUA kukarabati Jengo lililomilikiwa na Wajerumani ili kutumika kwa shughuli za Utalii, Mafunzo kwa Wanafunzi wa Shahada ya Utalii

Katika kuhakikisha Sekta ya Utalii inakua na kuleta tija hapa nchini, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), kupitia Ndaki ya Misitu, Wanyamapori na Utalii pamoja na Kurugenzi ya Miliki na Kazi kimeweza kukagua ukarabati wa jengo lililopo eneo la Morning Sight katika Safu ya Milima ya Uluguru. Jengo hili hutumika kwa shughuli za utalii.