Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kupitia kitengo cha SUA Innovation Hub, kwa kushirikiana na kampuni ya AQUILA EYES GROUP (AEG) ya Morogoro nchini Tanzania kwa udhamini wa “The Belt and Road Geospatial Information Training Center (BRGTC)” wamefanikiwa kuendesha mafunzo ya siku tatu ya kimataifa ya matumizi ya mifumo ya taarifa za kigeographia (GEOSPATIAL INFORMATION SCIENCE) katika kutambua na kutatua changamoto mbalimbali za upatikanaji wa taarifa na matumizi yake katika sekta mbalimbali nchini.