Serikali kushirikiana na SUA kutunza eneo la Utalii wa Kihistoria
Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Pauline Gekul amesema serikali kupitia Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika itaendelea kushirikiana na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kuyaendeleza, kukarabati na kutunza kumbukumbu zote za kihisitoria zilizoachwa na wapigania uhuru wa Afrika ya Kusini katika eneo la Kampasi ya Solomon Mahlangu.